shindano@dijitoframes.com

Dijito Challenge 25'

Je, wewe
ni mwanachuo
mjasiriamali ?

Shindano la Dijito 25' linakufaa

Mwisho wa Usajili

Tar 12 Oct 2025
Ona zaidi

Habari, Mwanachuo Mjasiriamali

Karibu kwenye shindano la Dijito 25’ linalowaunganisha wanafunzi wa vyuo vikuu nchini Tanzania ili kushindana, kujifunza na kuunda suluhisho bunifu za kijamii na kibiashara. Hii ni nafasi yako ya kukuza biashara yako na kuleta mabadiliko chanya katika jamii yako.

Kuhusu Shindano

Dijito 25’ ni shindano linalolenga kukuza vijana katika ujasiriamali kwa kidigitali, ubunifu wa bidhaa, na teknolojia. Washiriki wataelezea biashara zao zinatatua changamoto zipi katika jamii zao.

Washindi Watapata

-> Huduma bure ya graphics design & branding
-> Fursa ya mentorship kukuza biashara

JISAJILI SASA

Mtiririko wa shindano

Tunawawezesha vijana kwa maarifa na zana za ubunifu ili kubadili kukuza biashara na miradi yao. Kila shindano linawaunganisha wabunifu, mawinga, wajasiriamali na wanafunzi mbalimbali.

Hatua Ya Maombi

Maombi ya Dijito 25' Challenge yataanza tarehe 7 Oktoba 2025 hadi tarehe 12 Oktoba 2025. Unaweza kujisajili kupitia: Hapa

Hatua Ya Uhakiki

Baada ya dirisha la maombi kufungwa, maombi yote yatahakikiwa. Mchakato utajumuisha kuhakiki taarifa za biashara na kutathmini ubunifu wa biashara husika.

Kutangaza Washindi

Waombaji watakaofanikiwa kupita hatua ya uhakiki watachakatwa kupata wajasiriamali bora.

Zawadi

Wajasiriamali watakaoshinda watapata huduma ya bure ya graphics design kutoka Dijito Frames na fursa za ushirikiano siku za mbeleni.

Zaidi Kuhusu Sisi

Tumeanzishwa chini ya Dijito Frames kwa lengo la kujenga kizazi kipya cha wabunifu na wajasiriamali wanaotumia teknolojia kama chombo cha maendeleo. Kila mwezi tunazindua changamoto mpya inayolenga sekta tofauti kutoka ubunifu wa kidigitali hadi teknolojia ya kijamii.

Ungana Nasi

1205 Ilala,
Dar es Salaam,
Tanzania

Wasiliana Nasi

shindano@dijitoframes.com +255 756 990 474 +255 734 844 681